Taifa Leo | Kenya Live News
Sat
18
May
24
May 18, 2024 at 02:24PM
NA MWANDISHI WETU WATU tisa wamepoteza maisha Jumamosi asubuhi baada ya basi kuanguka katika Mto Mbagathi. Ripoti ya polisi katika kituo cha polisi cha Ongata Rongai ilisema dereva wa basi la sacco ya Naboka, ambalo lilikuwa likitoka eneo la Gataka kuelekea upande wa Karen jijini Nairobi, alipoteza udhibiti na likatumbukia mtoni. “Ajali ilitokea dakika 20 […]
May 18, 2024 at 01:46PM
NA MWANGI MUIRURI MBUNGE wa Gatundu Kusini Bw Gabriel Kagombe anasakwa na maafisa wa Idara ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai (DCI) kwa tuhuma za kuua na kujeruhi kwa risasi alipojipata katika mshikemshike wa kisiasa Thika Mjini mnamo Ijumaa. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Kiambu Bw Michael Muchiri, mtu mmoja aliaga dunia huku […]
May 18, 2024 at 01:15PM
NA OSCAR KAKAI MAMIA ya wasichana ambao wameokolewa kuepuka ukeketaji na ndoa za mapema wananufaika kwa kupata elimu katika Shule ya Wasichana ya St Elizabeth Morpus iliyoko Kaunti ya Pokot Magharibi huku wakipigana na mabadiliko ya tabianchi kwa kupanda miti. Shule hiyo mbali na kutoa elimu, hutumika kama kituo cha kuokoa wasichana wanaohangaishwa na minyororo […]
May 18, 2024 at 12:18PM
NA CHARLES WASONGA AZMA ya Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino ya kutwaa wadhifa wa Ugavana wa Nairobi mwaka 2027 imepigwa jeki kwa kupata uungwaji mkono kutoka kwa Mbunge wa Embakasi ya Kati Benjamin Gathiru almaarufu Mejja Donk. Kwenye kanda ya video inayosambaa mitandaoni, mbunge huyo aliyechaguliwa kwa tiketi ya chama cha United Democratic Alliance […]
May 18, 2024 at 11:39AM
NA MAUREEN ONGALA MWENYEKITI wa kamati ya mipangilio ya miji katika Bunge la Kaunti ya Kilifi amewashauri wenyeji na wakazi kujenga nyumba zao kwa mpango kuepuka hasara ya kufurushwa na kubomolewa makazi. Bw Raymond Katana, ambaye ni mwakilishi wadi ya Sokoni, amewataka wakazi kuhusisha idara husika wakati wa ujenzi huo kama njia ya kujiepusha na […]
May 18, 2024 at 10:55AM
NA MWANGI MUIRURI NAIBU Rais Rigathi Gachagua na Mbunge wa Kiharu, Bw Ndindi Nyoro wameibuka kama washindani wawili wa kujitafutia ushawishi wa siasa za Mlima Kenya. Swali linalosumbua wengi na kukanganya hata wanasiasa wa eneo hilo ni kuhusu ni nani hasa kati yao wawili anawafaa zaidi katika mkondo wa siasa za sasa na za baadaye. […]
May 18, 2024 at 10:53AM
NA MASHIRIKA MANCHESTER United inalenga kuwasilisha ofa nzuri ili kumtwaa mfungaji bora wa Aston Villa, Ollie Watkins. Watkins amekuwa wembe shoka la Aston Villa kufyeka wapinzani akiwasaidia kufuzu Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu ujao. Hata kabla mechi yao kutamatisha Ligi Kuu ya Uingereza (EPL), Villa tayari imejihakikishia kumaliza nambari nne ligini baada ya washindani wao […]
May 18, 2024 at 10:41AM
NA ROSELYNE OBALA KUKOSEKANA kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua wakati Rais William Ruto alimkaribisha mwenzake wa Uganda Yoweri Museveni katika ziara ya kiserikali ni mojawapo ya matukio tisa mfululizo ambayo yanaibua maswali kuhusu aliko kiongozi huyo anayeshikilia wadhifa wa pili wa juu nchini. Kwa kawaida, Wakenya wamezoea kumuona Bw Gachagua karibu na mkubwa wake katika […]
May 18, 2024 at 09:55AM
NA BRIAN OCHARO MAHAKAMA Kuu mjini Malindi imeamuru Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (ODPP) kupunguza mashtaka ya mauaji dhidi ya mhubiri mwenye utata Paul Mackenzie na washirika wake kutoka mashtaka 191 hadi 12 pekee. Jaji Mugure Thande alikubaliana na Mackenzie na washirika wake 29 kwamba mashtaka yalikuwa mengi sana na yatasababisha kucheleweshwa kwa […]
May 18, 2024 at 08:55AM
SAMMY WAWERU Na LABAAN SHABAAN HUKU sehemu nyingi nchini zikiendelea kushuhudia athari za mvua kubwa, mifumo kupitisha maji imezibwa na taka zilizosombwa. Mafuriko hayo yamesababisha uharibifu wa barabara na makazi. Uvumbuzi wenye ubunifu unahitajika ili kukabili hatari hii. Kampuni ya ujenzi, Bainridge Construction Company, ambayo ina utaalamu katika nyanja za ujenzi na uhandisi wa majengo inaongoza […]

Support Our Website

Ads help us keep our content on kenyalivetv.co.ke free for you. Please consider supporting us by disabling your ad blocker or whitelisting our site in your ad blocker settings.

You are currently offline.
You are back online.