To continue using the website, you must be logged in.

Your login information is stored on your browser only.

OR
Sun
27
Apr
25

Support Our Website

Ads help us keep our content on kenyalivetv.co.ke free for you. Please consider supporting us by disabling your ad blocker or whitelisting our site in your ad blocker settings.

Apr 27, 2025 at 07:54PM
KUKOSA kwa Bunge kupitisha sheria ya kudhibiti mashirika ya kidini kuwalinda Wakenya dhidi ya viongozi wa kidini wanaotoa mafunzo ya kupotosha kumechangia kuwepo kwa makundi ya kidini yenye misimamo mikali. Makundi haya yanaendelea kufanya shughuli zao ambapo katika kisa cha punde zaidi watu wawili waliripotiwa kufariki katika kanisa moja huko Migori. Mswada wa Mashirika ya Kidini wa Mwaka 2024, uliotokana na uchunguzi wa Seneti kuhusu mauaji ya Shakahola, ulilenga kudhibiti kuibuka kwa makanisa tata na kuyatoza ushuru kutokana na mapato ya sadaka na zaka. Hata hivyo, mswada huo haukuchapishwa kutokana na shinikizo kutoka kwa viongozi wa kidini walioupinga. Mswada huo ulipendekeza faini ya Sh5 milioni au kifungo cha hadi miaka mitatu jela, au adhabu zote mbili kwa wamiliki wa mashirika ya kidini ambayo hayajasajiliwa. Jumapili, Seneta wa Tana River Danson Mungatana, ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya muda ya Seneti iliyochunguza mauaji katika msitu wa Shakahola, alifichua kuwa mswada huo uliondolewa kutokana na malalamishi ya viongozi wa kidini. Hata hivyo, Seneta wa Makueni Dan Maanzo alipinga mswada huo akisema kuwa Kenya tayari ina sheria za kutosha kushughulikia uhalifu wa aina hiyo. [caption id="attachment_171294" align="alignnone" width="2000"] Kanisa tatanishi la Malkio St Joseph Mission of Messiah in Africa eneo la Opapo, Rongo, Migori. Picha|George Odiwuor[/caption] Uchunguzi wa Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) ulionyesha kuwa miili hiyo ilikuwa ya wafuasi wa Pasta Paul Mackenzie wa Kanisa la Good News International, aliyewahadaa wafuasi wake wafunge hadi kufa kwa njaa. Kufikia mwisho wa mwaka jana, zaidi ya miili 400 ilikuwa imetolewa kutoka kwa makaburi ya muda, huku zaidi ya watu 600 wakiendelea kuripotiwa kutoweka. Licha mauaji hayo serikali inaonekana kutojifunza lolote kutoka Shakahola, kwani wafuasi wawili wa kanisa la Melkio Saint Joseph Missions of Messiah Africa walifariki ndani ya kanisa baada ya kukataa kwenda hospitalini, kutokana na ushawishi wa kidini. Takribani waumini 57 wa kanisa hilo walikataa kurudi nyumbani wakisisitiza kuwa wangeendelea kukaa katika kanisani licha ya vifo hivyo. [caption id="attachment_155227" align="alignnone" width="500"] Miili iliyofukuliwa Shakahola ambapo wengi wa waathiriwa walikuwa watoto. Mhubiri Paul Mackenzie amehusishwa na vifo hivyo. Picha|Kevin Odit[/caption] Hadi sasa, hakuna mtu aliyeshtakiwa kuhusiana na vifo hivyo, huku hofu ikitanda kuwa shughuli za kanisa hilo zinaweza kufanana na za Shakahola. Ili kushughulikia ongezeko la mafunzo hatari ya kidini, mswada uliokuwa umependekezwa ulilenga kuanzishwa kwa Ofisi ya Msajili wa Mashirika ya Kidini (ORRO). ORRO ingesajili na kudhibiti mashirika ya kidini na kuhakikisha yanafuata sheria.uswada huo ulisema: “Mtu yeyote hataruhusiwa kuanzisha, kuendesha au kusaidia katika kuendesha shirika la kidini bila kusajiliwa kwa mujibu wa sheria hii.”
Apr 27, 2025 at 07:03PM
GOR MAHIA Jumapili ilinyeshea Mara Sugar 4-0 katika uga wa Dandora jijini Nairobi na kurejelea ushindi huku Tusker ikiponza nafasi ya kupaa kileleni mwa Ligi Kuu (KPL). Tusker, mabingwa mara 13, walipata pigo baada ya kupoteza uongozi wa 1-0 na kuchapwa 2-1 na Mathare United kwenye mechi ya mapema iliyosakatwa uga huo huo wa Dandora. Katika mechi nyingine Jumapili, Ulinzi Stars ilipata ushindi mkubwa huku ikiipiga FC Talanta 4-0 kwenye uwanja wa Ulinzi Sports Complex mtaani Lang’ata.  Katikati mwa wiki jana, FC Talanta iliwashangaza wengi kwa kupiga Gor Mahia 1-0 uwanjani Dandora. Aidha Kakamega Homeboyz iliponza nafasi ya kuendelea kupanda nafasi za juu KPL baada ya kuaga sare tasa dhidi ya Sofapaka kwenye uwanja wa Mumias Sports Complex, Kaunti ya Kakamega Ugani Dandora, Gor ilitawala mchuano huo na kuvuna ushindi mkubwa kupitia mabao ya Shariff Musa, Enock Morisson, Gideon Bendeka na Alpha Onyango. Kupata huku alama tatu kulikuwa kutamu ikizingatiwa Gor ilikuwa imepata sare ya 1-1 dhidi ya Sofapaka kabla ya kupigwa 1-0 na FC Talanta katikati mwa wiki Ushindi huo uliongeza  alama ambazo Gor imejikusanyia msimu huu hadi alama 50 baada ya mechi 28. Zikiwa zimesalia mechi sita msimu huu utamatike, Kenya Police inaongoza kwa alama 52 kisha Tusker ikiwafuata kwa alama 51. Kocha wa Gor Mahia Sinisa Mihic alikuwa amerejea kwenye benchi ya kiufundi baada ya kukosa mechi za Sofapaka na FC Talanta kutokana na marufuku aliyopigwa kwenye ushindi wa 1-0 dhidi ya KCB mnamo Aprili 7. Wikendi inayokuja, Gor itakuwa na kibarua kikali,  ikitarajiwa kupambana na nambari nne Shabana (alama 46) uwanjani Gusii, Kaunti ya Kisii. Ugani Dandora, mvamizi raia wa Uganda Deogratious Ojok aliwapa Tusker uongozi kipindi cha kwanza lakini Musa Masika akafunga mawili kwa Mathare United, moja kupitia mkwaju wa penalti na kupunguza kasi ya vijana wa Kocha Charles Okere ligini. Winga Boniface Muchiri, Meshack Karani, Amatton Samunya na Joseph Ochieng walifungia Ulinzi Stars mabao yao dhidi ya FC Talanta. Licha ya kuselelea eneo hatari la kushushwa ngazi kwa kipindi kirefu, Ulinzi sasa wapo nambari 11 kwa alama 35 baada ya mechi 29 huku FC Talanta ikiwa pabaya, nambari 15 kwa alama 29 baada ya mechi 29.
Apr 27, 2025 at 03:43PM
NDEGE ya KQ kutoka JKIA kwenda Dar es Salaam, Tanzania imeagizwa kurejea Nairobi dakika 25 baada ya kupaa kufuatia hofu ya kuvuja kwa kemikali hatari kwenye eneo la mizigo, wasafiri katika ndege hiyo wameripoti. Kulingana na ripoti hizo, ndege hiyo KQ484 tayari ilikuwa hewani wakati agizo lilipotumwa kwamba ipige kona na kurejea Nairobi mara moja huku abiria wakiambiwa kuna hatari kwamba bakteria aina ya Tuberclosis Bacilli huenda ilivuja kutoka kwa eneo la mizigo wakati wa safari ya awali. Abiria wameambiwa wasiondoke na maafisa wa afya wameingia kwenye ndege hiyo kuchukua maelezo yao. Eneo la mizigo limepuliziwa dawa na kufikia wakati wa kuandika taarifa hii, bado ndege hiyo haikuwa imeruhusiwa kuendelea na safari huku abiria wakianza kuzusha.
Apr 27, 2025 at 02:07PM
MKENYA Sebastian Sawe ameshinda London Marathon kwa saa 2:02:26 akimpita raia wa Uanda Jacob Kiplimo. Aidha, Mkenya Alexander Mutiso ambaye alibeba taji hilo mwaka jana amekuwa wa tatu katika mbio ambazo lejendari wa miaka mingi Eliud Kipchoge ameridhika na nafasi ya sita. Habari kamili ni hivi punde...
Apr 27, 2025 at 06:45AM
KOCHA wa Gor Mahia Sinisa Mihic Jumamosi  alikiri kuwa presha inaendelea kumlemea katika juhudi za  klabu ya kutetea taji lake la  Ligi Kuu (KPL). Mihic, 48 amekiri kuwa wakiendelea kudondosha alama, basi watajipata pabaya na kupoteza taji hilo ambalo Gor imelichukua mara 22. Mihic atarejea kwenye benchi ya kiufundi ya Gor Jumapili baada ya kukosa sare ya 1-1 dhidi ya Sofapaka na kupigwa 1-0 na limbukeni FC Talanta mnamo Alhamisi uga huo huo wa Dandora. Kocha huyo alipewa kadi nyekundi kwenye ushindi wa 1-0 dhidi ya KCB ndiposa hakuwa kwenye benchi katika michuano hiyo miwili. “Presha imezidi na sasa lazima tushinde mechi zetu kwa sababu kila kitu kinatuwia vigumu. Najua mashabiki wamevunjika moyo na sasa ni wajibu wa kila mtu kujituma uli tuyapate matokeo mazuri,” akasema Mihic. Kocha huyo alijizuia kuzungumzia uhasama ambao upo kwenye benchi ya kiufundi  huku baadhi ya mashabiki wakimtaka naibu wake Zedekiah ‘Zico’ Otieno aondoke klabuni humo. K’Ogalo iliipiga Mara Sugar 2-0 kwenye mechi ya mkondo wa kwanza Novemba 30 mwaka uliopita. Mashabiki wametoa onyo kuwa Gor isiposhinda Mara Sugar mnamo Jumapili, basi benchi ya kiufundi na wachezaji wajiandae kukimbia. Kenya Police inaongoza KPL kwa alama 52, huku Tusker ikivaana na Mathare United Jumapili ikilenga pia kurejea kileleni   Gor wakiwa na alama 47 wapo nambari tatu. RATIBA YA JUMAPILI JUMAPILI Kakamega Homeboyz v Sofapaka (Mumias Sports Complex, Kakamega 2pm) Ulinzi Stars v FC Talanta (Ulinzi Sports Complex, Nairobi 3pm) Mathare United v Tusker (Dandora, Nairobi, 1pm) Gor Mahia v Mara Sugar (Dandora, 4pm)
Apr 26, 2025 at 07:22PM
NDOTO ya Michelle Omondi ya kumaliza masomo yake upili katika Shule ya Wasichana ya Pangani nusura ikatizwe kutokana na ukosefu wa karo. Michelle, 15 anatoka familia maskini lakini sasa anaweza kufurahi baada ya shirika moja lisilo la kiserikali kumsaidia na kumpa udhamini wa masomo.Tineja huyo ni kati ya wasichana na wanawake 1, 544 ambao SHOFCO imewalipia karo ili wamalize masomo ya shule ya upili katika Kaunti ya Nairobi.“Kuna wakati ambapo nilifikiria ningeacha masomo na kuanza kusaka vibarua vya kusaidia familia yangu. Kulipiwa karo kumenisaidia sana na kunipa matumaini ya kusaka maisha bora,” akasema Michelle.Bi Maureen Isinga, mzazi katika Shule ya Wasichana ya Huruma, naye alisema mwanawe alikuwa na deni la karo lakini sasa anaweza kutabasamu baada ya Shofco kumlipia deni hilo na kugharimia elimu yake yote.“Hawajamlipia tu karo, pia wamelipa deni la awali ambalo lilikuwa likinisumbua. Sasa nitamakinika kusaka karo kwa watoto wangu wawili,” akasema Bi Isinga wakati Shofco ilizindua utoaji udhamini wa karo Nairobi.Wanafunzi kutoka kaunti mbalimbali ndogo ambao wanatoka familia maskini na ni werevu walinufaika kwa kulipiwa karo.Wakati wa hafla hiyo, Afisa Mkuu Mtendaji wa Shofco , Bw Kennedy Odede, alisema shirika hilo lina imani kuwa kupitia elimu, maisha ya familia nyingi maskini yataimarika.“Elimu inastahili kuwa haki na wasichana hawa wameonyesha ari na bidii masomoni licha ya kutatizwa na karo. Tunawekeza kwenye taaluma yao ya baadaye kupitia ufadhili huu ambao tunawapa,” akasema Bw Odede.Kati ya 1, 544 walionufaika, 159 walikuwa wasichana waliojifungua watoto na wamerejelea masomo ili kutimiza ndoto zao za kupata elimu.Shofco inalenga kuwasaidia zaidi ya wasichana 11,000 maskini kwa kuwapa udhamini wa masomo kote nchini.
Apr 26, 2025 at 07:13PM
KINARA wa upinzani, Raila Odinga Ijumaa aliwatetea magavana James Orengo (Siaya) na Prof Anyang’ Nyongó (Kisumu) ambao wamekuwa wakikashifiwa kwa kukosoa utawala wa Rais William Ruto, akisema wanazungumza kwa niaba yake na chama cha ODM. Bw Odinga alisema kuwa wawili hao hawafai kusulubishwa kwa kukosoa serikali, akisema wanasema ukweli na masuala waliyoyaibua yanahusiana na ugatuzi na lazima yatiliwe manani na serikali hii. “Orengo hajafanya kosa lolote la kiuhalifu na ana haki ya kuzungumza kwa sababu tuko katika taifa la kidemokrasia. Hakuna makosa akizungumza kuhusu maelewano na ushirikiano wetu na UDA, “Profesa Nyongó akiongea kuhusu ugatuzi anaongea kwa niaba ya ODM. Ugatuzi ndio muhimu zaidi katika katiba hii ambayo tuliandaa katika ukumbi wa Bomas,” akasema waziri huyo mkuu wa zamani. Alikuwa akizungumza wakati wa mazishi katika Kaunti ya Homa Bay ambako aliandamana na vigogo wa ODM akiwemo mwenyekiti wa chama Gladys Wanga. Kigogo huyo wa siasa za upinzani, alisema kuwa Kenya ni taifa la kidemokrasia na kwa kuzindua ushirikiano na Rais Ruto, hakumaanishi kuwa hawawezi kukosoa serikali au kuzungumza serikali inapokosea kisera. “Hatuna muungano wa kisiasa na UDA bali tuna ushirikiano nao ambapo baadhi ya wanachama wetu wanahudumu serikali na maelewano tuliotia saini hayamaanishi sisi sote tumeingia kwa serikali,” akaongeza. “Watu wasipige kelele eti Raila alisema hii na mtu mwingine amekataa kufuata. Hakuna mgongano wowote ambao unastahili kutokea serikali ikikosolewa,” akasema. Gavana Orengo amekuwa akikosolewa kutokana na matamshi ambayo alitoa mbele ya Rais Ruto na Bw Odinga eneobunge la Rarieda mnamo Aprili 12. Wakati wa mazishi ya msaidizi wa kibinfasi wa Raila marehemu George Oduor, Bw Orengo alisema hawezi kuwa kibaraka kwa kuwa maendeleo ni haki ya raia wala hawafai kuipokea kutokana na hisani ya serikali. “Mimi siwezi kuwa kibaraka kwa sababu tulipigania katiba ambayo watu wanaruhusiwa kuzungumza. Nilikuwa bunge ambalo wabunge walikuwa wakimwaambia Rais Daniel Moi kuwa hakuna mahali ataenda na angeongoza milele,” akasema Bw Orengo. “Mkiendelea kuwa vibaraka hatutakuwa na nchi. Waambieni viongozi wenu ukweli na mimi siimbi mtu kwa sababu lugha ambayo nimesikia hapa, inaashiria kuwa nchi hii inapoteza hadhi yake,” akasema Bw Orengo. Gavana huyo alikashifiwa na baadhi ya viongozi wakuu wa ODM huku wale wa mashinani Nyanza wakipendekeza madiwani wa Kaunti ya Siaya wamtimue kwa kumpinga Raila. Mnamo Jumatano, Profesa Nyongó naye alikuja juu juu na kurukia serikali ya Rais Ruto kuhusu kukwamilia fedha za ujenzi wa barabara akisema pesa hizo zinastahili kuwasilishwa kwa kaunti. Profesa Nyongó alisema kaunti zinasimamia vyema sekta ya afya kwa hivyo itamudu hata kusimamia ujenzi wa barabara. “Hatufai kukubali utawala huu uturejeshe nyuma na hatufai kuruhusu matunda ya mfumo wa ukombozi wa pili yapotee tu,” akasema Profesa Nyongó. Kujitokeza hadharani kwa Raila kutetea Profesa Nyongó na Orengo kunatarajiwa kutuliza shinikizo ambazo zimekuwa zikiwaandama. Baadhi ya viongozi wamekuwa wakidai wanatumiwa kuyumbisha serikali na kuwataka wakome ili eneo la Nyanza linufaikie kupitia miradi ya maendeleo. Baadhi ya wabunge wa ODM kama wa Homa Bay mjini Peter Kaluma, wamekuwa mstari wa mbele kumpapura Bw Orengo ambaye alipinga hatua ya ODM kujiunga na Rais Ruto katika kilele cha maandamano ya Gen Z mnamo Juni/Julai mwaka uliopita. Jana, Bw Odinga aliwaambia wafuasi wake wakae ange akisema kuwa mbele ni kuzuri wala hajazama kisiasa. “Simameni nami na tuwe pamoja na hapa mbeleni tutafika mahali ambayo tumekuwa tukilenga,” akasema kauli inayoweza kufasiriwa kuwa huenda akawania urais tena. Raila aliunga mkono msimamo wa Profesa Nyongó kuhusu fedha za ujenzi wa barabara akisema hela ambazo zinastahili kugharimia maendeleo, hazitolewi na serikali kuu. Kwa mara nyingine, alisisitiza kuwa Hazina ya Ustawi wa Maeneobunge (CDF)  lazima iondolewe mikononi mwa wabunge ili pesa hizo zipewe kaunti kufanyia maendeleo.
Apr 26, 2025 at 07:05PM
AFC LEOPARDS  Jumamosi ilisitisha rekodi duni ya kutopata ushindi kwenye mechi sita zilizopita huku Kenya Police ikirejea kileleni mwa Ligi Kuu (KPL) kupitia ushindi wa 2-1 dhidi ya KCB ugani Sportpesa Arena, Kaunti ya Murangá.   Ingwe ilinyorosha Bidco United 3-1 katika uga huo huo wa Dandora mechi ambayo ilianza saa 10 jioni. Shabana nao waliendelea kukwea jedwali la KPL, wakifunga Nairobi City Stars 2-0 uwanja wa Kenyatta, Kaunti ya Machakos. Kwenye mechi nyingine Kariobangi Sharks walikemewa na Kocha William Muluya wakipigwa 2-1 na Bandari katika uga wa Dandora. Murangá Seal ipo pabaya kuondolewa KPL mwishoni mwa msimu iwapo hawatayapata matokeo mazuri. Timu hiyo ilipigwa 3-2 na Posta Rangers kwenye mchuano uliogaragazwa pia katika uga wa Kenyatta. Ingwe haikuwa imepata ushindi kwa kipindi kirefu lakini mashabiki wao waliojaa ugani Dandora walijawa na tabasamu huku Christopher Koloti akifunga magoli mawili na Kennedy Owino akiongeza jingine. Bao la Bidco la kufutia machozi lilipachikwa wavuni na Simon Abuko. Ushindi huo uliwapaisha Ingwe, mabingwa mara 12 wa KPL, hadi nafasi ya tano kwenye msimamo wa jedwali la KPL kwa alama 41 baada ya mechi 28 Kenya Police waliipiku Tusker kileleni, wakiwa na alama  52 kutokana na mechi 28. Tusker wanacheza Jumapili dhidi ya Mathare United ugani Dandora na watarejea juu wakishinda. Mabao mawili ya Kenya Police dhidi ya KCB yalititigwa nyavuni na David Owino huku Patrick Otieno akifungia wanabenki hao. Zikiwa zimesalia mechi sita msimu ukamilike, KCB wapo nambari sita kwa alama 41. Tore Bobe iliendelea kujiandalia Gor Mahia wikendi ijayo, Keith Imbali na Darius Msagha wakihakikisha wananyanyasa City Stars ambao wanakumbwa na uchechefu wa kifedha na wapo mkia wa KPL. Shabana pia wanalisaka taji wakiwa nambari nne kwa alama 46, moja nyuma ya mabingwa watetezi Gor ambao wanavaana leo dhidi ya Mara Sugar ugani Dandora. “Waliingia kwa mtego wetu, tukajidhari wasitufunge na sisi tunalenga kufunga na kushinda mechi zetu. Hatujakutana na Gor na Tusker ambao wapo juu na lazima tuwashinde kwa hivyo, hata nasi tunawania ubingwa wa KPL,” akasema Kocha wa Shabana Peter Okidi.      
Apr 25, 2025 at 11:36AM
KATIBU wa Wizara ya Usalama, Raymond Omollo amewahimiza vijana kujisajili na Mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA) na kuipigia debe katika jamii zao. Kulingana naye, SHA ni kielelezo bora kuhusu jinsi sera ya kibunifu zinaweza kusuluhisha changamoto zinazokabili taifa na ulimwengu kwa jumla. Alisema Mamlaka hiyo ni moja kati ya miradi kabambe ya serikali inayodhamiriwa kufanikisha mabadiliko zaidi na imeundwa kwa namna ya kumwezesha kila Mkenya kupata huduma bora za afya pasipo kusambaratika kifedha. “Kwa miaka mingi, familia zimelazimika kufanya harambee au kuuza ardhi ili tu kumudu kugharamia matibabu. Hayo yatafika kikomo na SHA,” alisema Dkt Omollo Jumatatu katika warsha ya ngazi za juu ya vijana Kisumu. “Kama una mapato unachangia kiasi kidogo. Kama hauna, serikali inaingilia kati. Ni rahisi hivyo.” Kando na kutoa bima ya huduma za afya, Dkt Omollo alisema SHA itawezesha vilevile kuunda nafasi za kazi katika sekta ya afya ikiwemo huduma ya afya kwa jamii, matibabu kupitia simu, afya ya akili, biashara kuhusu afya bora na ubunifu unaohusu afya kidijitali. Aliwahimiza vijana kujisajili na pia kuwa mabalozi wa vuguvugu la SHA katika jamii zao akisisitiza kwamba Mamlaka hiyo ni “zaidi ya kupata matibabu.” “Ni mkondo unaowezesha hadhi kiuchumi na kuwapa vijana nafasi ya kujenga taaluma huku wakilinda maisha,” alisema. Alipuuzilia mbali alichotaja kuwa “habari za kupotosha kuhusu SHA” akitahadharisha vijana dhidi ya “kulaghaiwa na dhana zinazochochewa kisiasa, propaganda na uvumi.” “Amini vituo rasmi. Ulizeni maswali. Shirikisha. Lakini usiruhusu uongo ukunyime maendeleo,” alisema. Alisifu ubunifu, uwezo na ustahimilifu wa vijana Wakenya lakini akasisitiza ni sharti wajikakamue ili wapige hatua. “Tuna kizazi cha watu wachanga wenye maono. Lakini ahadi hiyo ni sharti iambatane na nidhamu, ukakamavu na ujasiri.” “Kuwa mchanga sio sababu. Ni manufaa. Yatumie kwa busara. Shughuli zina anayeziunga mkono, ni wakati wa kusonga mbele.” Kuhusu uongozi, Dkt Omollo alifafanua kinachohitajika zaidi ni kusuluhisha matatizo badala ya siasa na kushikilia tu afisi za umma. “Ni kuhusu kuanzisha biashara ya afya, kilimo biashara, kuendesha Sacco ya bodaboda, au kuwapa mwongozo wenzenu. Kuna njia nyingi za kuongoza na kenya inazihitaji zote.” Alisema barabara kuu ya kidijitali na nyumba za bei nafuu, kando na kuwa mipango ya maendeleo, ina umuhimu zaidi kwa kuunda ajira akihimiza vijana kuambatisha ujuzi wao na miradi ya kitaifa inayopatiwa kipaumbele. “Inahusu kukabiliana ana kwa ana na ukosefu wa ajira. Sio tu kusambaza intaneti na makazi.” Warsha hiyo ilileta pamoja makundi ya vijana, wafanyabiashara wa mashinani, viongozi wa jamii na wasimamizi kutoka Kisumu. Katibu alitoa ufadhili wa Sh500,000, matatu, pikipiki 10, tuktuk tano huku akisisitiza kwamba serikali imejitolea kuunga mkono miradi ya vijana na wanawake mashinani kupitia ufadhili na kuwaimarisha kiuchumi. Alisema badala ya kuangazia tu malengo ya kitaifa, mtindo wa uongozi wake Rais William Ruto unapatia kipaumbele vijana na kuboresha maisha mashinani kupitia mpango wa maendeleo kutoka mashinani (BETA). Alitaja nyumba za bei nafuu, teknolojia ya dijitali, mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya hali ya anga, kilimo na MSME, kuwa mipango inayoendeshwa na serikali inayolenga vijana. “Sekta hizi zimeteuliwa kwa makini kwa sababu zinaashiria nyanja muhimu ambazo hazitatumiwa kikamifu nchini. Zinaonyesha jinsi vijana wetu wanaweza kuongoza, kuunda ajira na ubunifu,” alifafanua. “Serikali inatekeleza wajibu wake kwa kuunda miundomsingi, kuongeza ufadhili, kuzindua tasnia za kidijitali na kondoa vikwazo. Lakini sasa tunahitaji nguvu za vijana. Tunahitaji maarifa, ujuzi na ari yenu.”
Apr 25, 2025 at 10:55AM
HIVI mbona tusionyeshe heshima, angaa kidogo tu, hata ‘tunapovuna’ na kuuza figo za watu? ‘Unapoivuna’ yangu bila kuniambia, halafu unaipandikizia mgonjwa asiyejua ni ya kuibwa, umeniachaje? Angalau ungeniachia mwanya mdogo wa kujua ‘umenipunguza’ ili nami nitafute huko mitaani ni nani anayetembea na figo ya kuibwa bila taarifa. Nikipata fursa ya kukutana na aliyenufaika na figo yangu ninaweza ama kuamua kumwachia, hasa kwa kuwa moja inanitosha, au nimfunze kikwetu. Ninakotoka, na hapa nazungumza kama mjukuu wa mfugaji, tukipata mtu na ng’ombe wa kuibwa, kawaida tunamswaga ng’ombe huyo hadi zizini mwetu, kesi baadaye! Fikra hii inatokana na ukweli kwamba mwizi wa ng’ombe amenichosha sana nikimtafuta, hivyo wewe uliyeuziwa unaweza nawe kuchoka ukimfuata aliyekuuzia ili akurejeshee pesa zako. Muhimu zaidi ni ujifunze kuthibitisha vitu kabla ya kuvinunua kwa sababu vikiwa vya kuibwa, wewe na mwizi mnanyolewa kwa wembe mmoja. Hata kisheria, anayepatikana na mali ya wizi huchukuliwa kuwa mwizi pia na kuadhibiwa ipasavyo kwa maana ndiye anayembunia mwizi soko. Hata hivyo, kwa kuwa tumeumbiwa utu, katika kisa cha figo na sehemu nyinginezo, nawasihi wezi wazingatie kwamba hata nikikutana na mtu akiwa na figo yangu, siwezi kuing’oa kama mche na kwenda nayo nyumbani. Nitamrai anirejeshee, na akinisadikisha kwamba anaitegemea sana, labda nitamwambia anunue chai tu tumalize maneno hayo badala ya kuwahusisha polisi. Makubaliano ya aina hii humsaidia aliyeathiriwa na wizi, na aliyenufaika na wizi pia. Mwizi naye? Laana anayo tayari kwa sababu sehemu hizo muhimu hazipandwi shambani, ni zawadi ya Mungu. Kisa cha Hospitali ya Mediheal kushukiwa kwamba inaiba na kuuza figo za watu kimenikumbusha kitu nilichoambiwa na rafiki yangu wa dhati nilipohamia Amerika. Nilitahadharishwa kwamba nikijaza fomu ya kuomba leseni ya kuendesha gari, nisijaze chochote katika sehemu inayokuomba uwaruhusu ‘kuvuna’ sehemu zako za mwili. Alinishtua aliponieleza kuna matajiri wengi ambao wamelazwa hospitalini wakisubiri kupandikizwa sehemu kadha, kama vile moyo na figo, kwa hivyo ajali ikitokea, nionyeshe dalili za kutaka kutangulia ahera, ‘nitavunwa’ upesi! Tangu hapo, kila nikijaza fomu hiyo, kitu cha kwanza huwa kuziba sehemu inayoniomba nikubali ‘kuvunwa’ ili nisiijaze kimakosa nikaishia kuwa bidhaa. Watu si wema aisee! ‘Wavunaji’ wa Kenya wanapaswa kuwa na fomu za kujazwa, angaa tujue wanahitaji vitu hivyo ili tuwe waangalifu zaidi, tusiibiwe. Wakenya wengi wanauliza: Katika uchumi uliozorota hivi, kuna haja gani kuwa na figo mbili, mapumbu mawili, macho mawili na kadhalika ikiwa sehemu moja ya hizo inaweza kutumika bila matatizo? Tunapaswa kuwaita watu kama hao wafadhili uchumi, si wahujumu uchumi. Kwa hivyo? Haidhuru kuwatungia sheria ya kuwadhibiti na kuwasaidia ‘wasijivune’ wakiwa hai mpaka waishe. mutua_muema@yahoo.com
You are currently offline.
You are back online.